Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Tuesday, February 28, 2017

FAMILIA YASUSIA MAITI MKOANI GEITA YATAKA MARIDHIANO NA JESHI LA POLISI.


ge1
Baaadhi ya ndugu wa marehemu wakiwa wameketi kwa masikitiko wakisubilia muafaka wa kuzikwa kwa ndugu yao.
ge2
Kamanda wa Polisi Mkoani Geita Mponjoli Mwabulambo akikiri kutokea kwa tukio hilo mbele ya waandishi wa habari.
ge3
Wanafamilia wakiwa kwenye masikitiko.
    IMEANDALIWA NA MADUKA ONLINE.
Famili ya mzee Isaya Neligwa wa Mto wa Mbu Mkoani Arusha  imesusia kuchukua maiti ya Jeremia Isaya ambayo imehifadhiwa kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita ,huku wakidai kupata maridhiano na jeshi la polisi kwani ajali hiyo ilisababishwa na  gari ya polisi yenye nambari za usajili PT 4026 iliyomgonga na kusababisha  kifo chake.
 Tukio hilo la ajali lilitokea tarehe 12 mwezi wa pili majira ya saa 12:30 jioni  Kwenye eneo la Mwatulole kata ya Buhalahala ambapo gari la kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) likitokea Kasamwa kuja mjini Geita lilimgonga kijana huyo wakati alipokuwa akivuka barabara kwanda upande mwingine.
 Moja kati ya wanafamilia ,Bw Elineema Mafie,akizungumza ,amesema kuwa msaidizi wa  mkuu wa kitengo cha usalama barabarani alimpigia simu  jana na kumwambia kwamba suala  hilo jeshi la polisi  halihusiki na kwamba kutokana na maelezo hayo kutoka kwa polisi na kugoma kukaa na kuzungumzia mwafaka wa jambo  hilo wamegoma kuzika na kwamba hadi pale serikali itakapoingilia kati.
 “Sisi kama familia tumesikitishwa na kitendo cha polisi kumemgonga kijana wetu na ushahidi tunao lakini jambo la kusikitisha msaidizi wa mkuu wa kikosi cha usalama barabarani Mkoani hapa alinipigia simu jana na kuniambia kuwa  wao hawahusiki na suala  hili sisi tunasema kuwa hatuna ugomvi na Polisi nadhani ni vyema tukae nao na kufanya mazunmgumzo ambayo yatatoa  mwafaka wa jambo hili kama watagoma sisi hatutazika hadi pale serikali itakapoingilia kati”Alisema Mafie.
 Baba wa Marehemu,Mzee Isaya Neligwa, ameelezea kuwa taarifa za kijana wake kufariki alizipata kutoka kwenye mtandao wa kijamii wa whatsapp kuwa kijana wao amefariki kwa kugongwa na gari na kutokana na hiyo taarifa ilibidi wafatilie kujua kama kuna ukweli wa habari ya kijana wake kupoteza uhai.
 “Kuna Binti ambaye yupo Dar es salaam aliona kwenye mtandao wa whatsapp kuwa mzazi au ndugu wa Jeremiah anatafutwa na kwamba kijana huyo amefariki na kutokana na kwamba na yeye alikuwa ni mkazi wa mto wa mbu ilibidi atume ndugu zake waje wanipe taarifa na baada ya kufika tuliwasiliana na Binti ndipo aliponipa maelekezo ya kufika kwenye hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Geita na nilipofika nilishuhudia kuwa ndio yeye kiukweli nina masikitiko makubwa sana kutokana na tukio hili”Alisema Mzee Neligwa kwa masikitiko
 Kamanda wa Polisi Mkoani Geita,Mponjoli Mwabulambo ,alikiri  kutokea kwa tukio hilo na kwamba  wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo huku wakimshikilia askari aliyekuwa akiendesha gari hilo aliyefahamika kwa jina la Kosntebo Daniel.
 Mwili wa Jeremiah Isaya ambao hadi sasa upo katika chumba cha  kuhifadhia maiti kwenye hospitali  ya rufaa ya Geita,kwa siku 17 tangu afariki Dunia na hakuna mwafaka ambao umekwisha kupatikana kutoka kwa ndugu na jeshi la Polisi Mkoani Hapa.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment