Writen by
sadataley
6:03 PM
-
0
Comments
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani, John Kerry, ambaye alialikwa kuhudhuria mazungumzo hayo siku ya ijumaa amesema hawajafikia makubaliano kwani bado kuna mambo muhimu ambayo hayajakubaliwa.
Lakini bado kuna matumaini huenda pande hizo zikafikia hatua muhimu licha ya changamoto zinazowakabili katika kufikia muafaka utakaoridhiwa na pande zote.
Waziri wa mambo ya nje wa Urusi, Sergei Lavrov anatarajiwa kuwasili mjini Geneva jumamosi hii kushiriki mazungumzo hayo.
Kuwasili kwa Lavrov kutawakutanisha Mawaziri wa mambo ya nje wa mataifa yote sita yenye nguvu ambayo kwa takribani muongo mmoja yamekuwa yakizozana na Tehran juu ya mpango huo.
Mataifa ya magharibi yamekuwa yakiishuku Iran kutafuta uwezo wa kutengeneza silaha za nyuklia lakini Tehran imekuwa ikikanusha na kusema kuwa lengo lao ni matumizi salama pakee.
Lakini bado kuna matumaini huenda pande hizo zikafikia hatua muhimu licha ya changamoto zinazowakabili katika kufikia muafaka utakaoridhiwa na pande zote.
Waziri wa mambo ya nje wa Urusi, Sergei Lavrov anatarajiwa kuwasili mjini Geneva jumamosi hii kushiriki mazungumzo hayo.
Kuwasili kwa Lavrov kutawakutanisha Mawaziri wa mambo ya nje wa mataifa yote sita yenye nguvu ambayo kwa takribani muongo mmoja yamekuwa yakizozana na Tehran juu ya mpango huo.
Mataifa ya magharibi yamekuwa yakiishuku Iran kutafuta uwezo wa kutengeneza silaha za nyuklia lakini Tehran imekuwa ikikanusha na kusema kuwa lengo lao ni matumizi salama pakee.
No comments
Post a Comment