Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, August 5, 2016

ANC yatarajia matokeo mabaya ya uchaguzi

Huku matokeo ya mwisho ya uchaguzi wa kimaeneo yakitarajiwa kutolewa leo, imebainika wazi kuwa chama cha ANC kimeibuka na matokeo mabaya zaidi ya uchaguzi kuwahi kushuhudiwa. Chama cha Democratic Alliance kimeibuka na ushindi mkubwa na muhimu katika baraza la manispaa ya Nelson Mandela Bay. Chama cha ANC kinajitahidi kuchukua udhibiti wa miji ya pretoria na Johannesburg. Hata hivyo, ANC inasalia kuwa chama maarufu katika siasa za Afrika Kusini, kwa kuzoa aslimia 54 ya kura hizo. Chama cha Democratic Alliance, kimekuwa kikiungwa mkono na wazungu pamoja na chotara, japo wapiga kura weusi wameanza kukiunga mkono, kwa kukatishwa tamaa na mwendo wa kobe wa uimarishaji wa uchumi wa chama tawala cha ANC, na sakata nyingi zinazomkabili rais Jacob Zuma.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment