Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, February 29, 2016

KKK lawashambulia weusi kwa visu California

Watu watatu wamedungwa visu katika mapigano kati ya kundi linalowachukia watu weusi la Ku Klux Klan (KKK) na waandamanaji wanaowapinga katika jimbo la California. Tukio hilo lilitokea karibu na eneo kulikopangwa mkutano wa hadhara wa wazungu wao wanachama wa KKK. Watu wanne walitiwa mbaroni katika makabiliano hayo, akiwemo mwanachama mmoja wa KKK aliyemdunga mweusi kisu. Msemaji wa polisi alieleza kuwa shida ilianza wakati wanachama wa KKK waliwasili katika uwanja wa Anaheim, karibu kilomita 50 Kusini Mashariki mwa Los Angeles, karibu na Disneyland. Msemaji wa polisi alisema kuwa wanachama hao wa KKK walishambuliwa weusi walipokuwa wanatoka kwenye gari. Mmoja aliangushwa chini. Waandamanaji watatu wanaopinga KKK walidungwa visu katika makabiliano hayo. Mtu mmoja aliyeshuhudia matukio hayo alisema kuwa wanachama wa KKK walikuwa wamelemewa. Mmoja wa waliodungwa visu anaugua na amelazwa hospitalini.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment