Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, March 20, 2015

Mancity kumtema Yaya Toure na wengine

Mabingwa wa ligi ya Uingereza Manchester City watamuuza Yaya Toure msimu huu katika mpango unaolenga kuwauza wachezaji wengine wa kilabu hiyo kwa lengo la kununua wachezaji chipukizi watakaoongozwa na mchezaji Kevin De Bruyn wa Wolfsburg. Kushindwa kwa kilabu hiyo na Barcelona katika mechi ya kufuzu kwa robo fainali ya kombe la vilabu bingwa Ulaya kumethibitisha kwamba mabadiliko makubwa yanahitajika katika kilabu hiyo. Katika wachezaji kumi na moja walioanzishwa katika mechi dhidi ya Barcelona ni Sergio Aguerro mwenye umri wa maka 26 aliye chini ya umri wa miaka 27. Huku Aguerro,Joe Hart,Vincet Kompany,Fernandinho na David Silva wakiwa na maisha marefu katika kilabu hiyo ,waliosalia huenda wakauzwa. Hii inamaanisha kwamba Yaya Toure,Bacary Sagna,Martin Demichelis,Alkesandar Kolarov ,Samir Nasri na James Milner ambaye kandarasi yake inaisha hatma yao haijulikani. Kati ya wachezaji ambao hawakuanzishwa katika uwanja wa Nou Camp siku ya jumatano usiku,Gale Clichy,Pablo Zabaleta,Jesus Navas,Fernandinho,Steven Jovetic na Edin Dzeko huenda pia wakauzwa. Frank lampard amesema kuwa anaondoka ili kujiunga na kilabu ya New York City nchini Marekani.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment