Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, March 20, 2015

J Goodluck:Tutalimaliza Boko Haram

Rais wa Nigeria, Goodluck Jonathan amesema ana matumaini kwamba katika muda wa mwezi mmoja kundi la wapiganaji wa kiislamu Boko Haram halitodhibiti sehemu yoyote. Wanamgambo hao waliokiri ushirikiano na kundi la Islamic State liliziteka sehemu kubwa ya eneo la kaskazini mashriki mwa Nigeria. Lakini operesheni ya kieneo imesadia serikali kudhibiti miji na vijiji kadhaa. Rais Jonathan anayewania kuchaguliwa tena katika siku nane zijazo ametetea jitihada zake za kukabiliana na ukosefu wa usalama na amesema anaamini atashinda katika uchaguzi huo. Kiongozi huyo amesema Boko Haram linazidi kuwa dhaifu na litasamabaratishwa. Ameeleza kwamba silaha mpya ilizopata nchi hihyo pamoja na ushirikiano na nchi jirani zimesaidia kuwasukuma wanamgambo hao nje ya miji na vijiji. Alipoulizwa ni wapi walikokimbilia, alieleza kwamba wakati wengi wamemiminika katika mipaka ya nchi hiyo, anadhani wengine wamekimbilia katika msitu wa Sambisa ulio ngome yao kaskazini mashariki mwa Nigeria.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment