Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, January 30, 2015

Umoja wa Afrika: mshikamano dhidi ya Boko Haram

    
Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika Nkosazana Dlamini-Zuma ametangaza mjini Addis Ababa, Ethiopia kuundwa kwa kikosi cha kimataifa kwa kuanzisha vita dhidi ya Boko Haram.
Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika Nkosazana Dlamini-Zuma ametangaza mjini Addis Ababa, Ethiopia kuundwa kwa kikosi cha kimataifa kwa kuanzisha vita dhidi ya Boko Haram.
AFP/ISSOUF SANOGO

Na RFI
Uamzi wa pamoja umechukuliwa na Umoja wa Afrika wakati wa kikao chake cha Baraza la amani na usalama Alhamisi Januari 29 jioni mjini Addis Ababa, Ethiopia na kuhudhuriwa na zaidi ya marais kumi na tano.

Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan na rais wa Cameroon Paul Biya hawakushiriki kikao hicho. Umoja wa Afrika unaunga mkono kikosi cha kimataifa cha wanajeshi 7500.
Lengo la Umoja wa Afrika ni kushawishi Umoja wa Mataifa kufadhili mashambulizi ya kikosi hicho cha Umoja wa Afrika.
Uamzi huo umechukuliwa na marais na viongozi wa serikali za Afrika Alhamisi 29 Januari mjini Addis Ababa, ambao wanakabiliwa na tishio la Boko Haram.
Mwezi ujao, Umoja wa Afrika utakutana rasmi na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, ili kuliomba kusaidia, kupitia mfuko wa amani, msaada wa vifaa na fedha kwa kikosi cha kimataifa chenye wanajeshi 7500, ambao watatakiwa, kwa mujibu wa mwenyekiti wa Umoja wa Afrika, Nkosazana Dlamini-Zuma, kupambana dhidi ya Boko Haram.
Umoja wa Afrika unaunga mkono jitihada za jumuiya ya nchi zinazochangia Ziwa Chad, za kuundwa kwa kikosi cha kimataifa kutoka Nigeria, Chad, Cameroo, Niger na Benin.
Uamzi huu umechukuliwa na zaidi ya marais kumi na tano ambao ni wajumbe wa Baraza la amani na usalama, uamuzi ambao unatazamiwa kupitishwa katika mkutano mkuu wa marais na viongozi wa serikali ambao utadumu siku mbili kuanzia Ijuma wiki hii.
Nigeria na majirani zake wameafikiana juu ya msimamo wa pamoja, baada ya miezi ya kutoaminiana na kutokuelewana. Lakini kama Umoja wa Afrika, kupitia jumuiya ya nchi zinazochangia ziwa Chad, una wanajeshi, bao unakabiliwa na ukosefu wa vifaa vya kijeshi na fedha.
Chanzo:http://www.kiswahili.rfi.fr
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment