Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Sunday, January 26, 2014

Ukraine:Upinzani wapata afueni

Rais wa Ukraine Victor Yanukovych ameupa upinzani baadhi ya nyadhfa muhimu za serikali katika juhudi za kumaliza maandamano ambayo yamekuwa yakiendelea nchini humo kwa majuma kadhaa sasa.
Shinikizo zamfanya Rais Victor Yanukovych kujumuisha upinzani katika serikali yake
Lakini viongozi hao wa upinzani wamesema kuwa hawako tayari kuchukua nyadhfa hizo huku makabiliano kati ya waandamanaji na polisi yakiendelea katika mji mkuu wa Kiev.
Kiongozi wa chama cha Ukrain Fatherland Arseniy Yatsenyuk amesema kwamba yeye na viongozi wengine wa upinzani wako tayari kuichukua serikali,lakini akasisitiza kuwa uamuzi huo utafanywa na wapiga kura na wala si rais.
Muhariri wa maswala ya kibiashara katika gazeti la Kiev post Mark Rechkevych amesema kuwa wapinzani hao hawakutaka kuhalilisha mamlaka ya rais huyo.
Upinzani umekuwa ukisisitiza kufanyika kwa uchaguzi wa mapema.
Wakati huohuo waandamanaji wamelizunguka jumba moja mjini Kiev ambapo polisi wa kukabiliana na ghasia wamewekwa.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment