Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, January 27, 2014

Tunisia yapata katiba mpya

Bunge la Tunisia limeidhinisha katiba mpya,ikiwa ni ya kwanza tangu kuondolewa madarakani kwa aliyekuwa rais wa taifa hilo Ben Ali, yapata miaka mitatu iliopita.
Hii ni katiba ya kwanza kuidhinishwa tangu Ben Ali kuondolewa madarakani
Spika wa bunge hilo Mustapha Ben Jaafar ameitaja katiba hiyo kama mojawapo ya makubaliano yaliyoafikiwa kwa mustakabali mwema wa Tunisia.
Mwandishi wa BBC nchini humo anasema kuwa wanasiasa wana imani ya kutuma ujumbe wa udhabiti na umoja kwa raia wa taifa hilo pamoja na jamii ya kimataifa.
Wakati huohuo waziri mkuu nchini humo Mehdi Jomaa amesema ameunda serikali mpya.
Baraza la mawaziri linashirikisha wataalam na watu wasioegemea upande wowote wa kisiasa, linatarajiwa kuongoza serikali hadi uchaguzi mpya utakapofanyika.
Mehdi Jomaa alichaguliwa kama waziri mkuu mnamo mwezi Disemba,baada ya serikali ilikuwa ikiongozwa na chama cha Ennahda kukubali kujiuzulu kufuatia ongezeko la hali ya wasiwasi kati yake na upinzani wenye misimamo wa kadri.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment