Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, January 24, 2014

Mlipuko mkubwa watikisa Cairo

Maafisa wa Misri wanasema kuwa kumetokea mlipuko mkubwa wa bomu nje ya Makao makuu ya polisi jijini Cairo ambapo watu wanne wamefariki na wengine zaidi ya 70 kujeruhiwa.
Mlipuko umetokea wakati wa kuadhimisha siku ya kuondolewa mamlakani kwa Hosni Mubarak
Kituo cha televisheni cha Serikali kimesema kuwa milio ya risasi ilisikika mara tu baada ya mlipuko huo.
Moshi ulionekana ukifuka juu ya majengo katikati mwa mji na picha za televisheni zilionyesha uharibifu mkubwa wa majengo hayo.
Zaidi ya ambulansi 30 zimepelekwa eneo hilo kushughulikia waathiriwa. Mlipuko huo umetokea siku ya kuadhimisha miaka mitatu tangu kupinduliwa kiongozi wa nchi hiyo Hosni Mubarak.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment