Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Sunday, January 26, 2014

Hakuna aliyesitisha mapigano Sudan-K

Serikali ya Sudan Kusini na wapiganaji wanaendelea kulaumiana kwa kuvunja makubaliano ya kusitisha mapigano ambayo yalianza kutekelezwa Ijumaa.
Wanajeshi wa serikali ya Sudan Kusini
Msemaji wa waasi, Brigedia Jenerali Lul Ruai, alieleza kuwa wanajeshi wa serikali wameshambulia maeneo yao katika sehemu kadha.
Serikali ilikanusha hayo na iliwalaumu waasi kwa mashambulio.
Kila upande unasema haufikiri kuwa upande wa pili unaweza hasa kudhibiti majeshi yake.
Maelfu ya watu wamekufa katika vita hivyo baina ya jeshi la serikali ya Rais Salva Kiir na wanajeshi watiifu kwa naibu wake wa zamani, Riek Machar.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment