Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, November 28, 2013

Waziri Mkuu wa Latvia ajiuzulu


Waziri Mkuu wa wa Latvia, Valdis Dombrovskis, amejiuzulu kufuatia kuporomoka kwa jengo moja nchini humo, Alhamisi iliyopita na kusababisha watu wapatao hamsini kuuawa.
Valdis Dombrovskis,waziri mkuu wa Latvia
Bwana Dombrovskis amesema amekubali kuwajibika kisiasa kutokana na mkasa huo ambapo paa ya duka moja kubwa la bidhaa katika mji mkuu, Riga, lilipinda na kuporomoka.
Polisi wameanzisha uchunguzi wa kihalifu kubaini kama taratibu za ujenzi wa jengo hilo zilizingatiwa au la; bustani ilikuwa ikijengwa juu ya paa la jengo hilo la maduka wakati ajali hiyo ikitokea.
Latvia imekuwa na siku tatu za maombolezo kuwakumbuka waathirika wa janga hilo, ambalo ni baya kuwahi kutokea nchini Latvia, tangu nchi hiyo ijipatie uhuru wake mwaka 1981.
Kujiuzulu kwa Bwana Dombrovskis, ambaye ameiongoza Latvia katika kipindi cha mgogoro wa kiuchumi, kumekuja wiki kadhaa kabla ya nchi hiyo kujiunga na umoja wa Ulaya.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment