Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, November 4, 2013

Washukiwa wa ugaidi mahakamani Kenya

Wanaume wanne wamefikishwa mahakamani nchini Kenya baada ya kuhusishwa na shambulizi la kigaidi lililofanyika dhidi ya jengo la Westgate nchini Kenya mwezi Septemba.
Magaidi wlaivamia Westgate kwa siku nne na kuwashika mateka wakenya waliokuwemo ndani ya jengo hilo wakati wa shambulizi hilo
Wanne hao wote walikanusha mashitaka hayo ikiwemo kosa la kuingia nchini bila vibali halali pamoja na kumiliki stakabadhi bandia za kujitambulisha.
Mahakama imeamuru wawekwe rumande.
Kundi la kigaidi la Somalia, Al Shabaab lilikiri kufanya shambulizi hilo la kigaidi ambapo zaidi ya watu sitini waliuawa.
Wanne hao walishitakiwa kwa kosa la kuhusika na shambulizi hilo la kigaidi ingawa hakuna hata mmoja alikuwemo ndani ya Jengo la Westgate wakati wa shambulizi hilo.
Wanne hao raia wa Somalia ni Mohammed Ahmed Abdi, Liban Abdullah, Adan Adan na Hussein Hassan.
Washukiwa hao ambao hawakuwa na mawakili walizuiliwa rumande kwa wiki moja baada ya kiongozi wa mashitaka kuomba muda zaidi kufanya uchunguzi.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment