Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, November 22, 2013

Rais wa Nigeria augua akiwa London

Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan
Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan
Nigeria imesema rais Goodluck Jonathan ameugua akiwa London na ameshauriwa kupumzika kwa siku kadhaa.

Taarifa kutoka ofisi ya rais imesema bwana Jonathan alitakiwa kuhudhuria mkutano wa uwekezaji katika mji mkuu wa Uingereza Alhamis lakini hakuweza kushiriki.

Taarifa hiyo imeongeza kuwa hali ya rais Jonathan si mbaya sana lakini imebidi tahadhari ichukuliwe na anapewa matibabu.

 Rais huyo wa Nigeria alifikisha umri wa miaka 56 wiki hii. Ameshika wadhifa wa urais wa Nigeria tangu mwaka 2010. Nchi hiyo ni maarufu kwa uzalishaji wa mafuta barani Afrika.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment