Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, November 22, 2013

Iran: Marekani yatishia vikwazo vipya

Kiongozi wa kidini wa Iran Ayatollah Khamenei
Afisa mmoja mwandamizi wa chama cha Democrat nchini Marekani, senata Harry Reid, amesema kuwa baraza la senate litaiwekea Iran vikwazo vipya mwezi ujao, iwapo mazungumzo yanayoendelea mjini Geneva, kuhusu mpango wake wa nuklia hayatafualu.
Wajumbe kutoka mataifa sita yenye ushawishi mkubwa duniani, ikiwemo Marekani, zinajaribu kuafikia mkataba wa awali ambao utawala wa Tehran utasaini kuidhinisha kupunguza urutubishaji wa madini ya uranium ili jamii ya kimataifa ilegeze baadhi ya vikwazo vilivyoiwekea.
Lakini baadhi ya masineta wanasema wana wasi wasi kuwa mkataba huo hautotosha kudhibiti mpango huo wa Iran.

Baada ya siku mbili za mazungumzo mjini Geneva, mjumbe mmoja wa Iran alisema kuwa maswala muhimu yangali kujadiliwa wakati mjumbe mwingine akisema kuna umuhimu wa kuondoa kile anachosema ni vizingiti vinavyotatiza mazungumzo hayo.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment