Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, November 29, 2013

KWAYA YA KWETU PAZURI WAKO NCHINI ZAMBIA

Ambassadors of Christ wakiimba katika tamasha la pasaka jijini Mbeya mapema mwaka huu.

Kwaya ya Ambassadors of Christ kutoka Kigali nchini Rwanda maarufu kama Kwetu Pazuri wapo nchini Zambia kwa ziara ya siku tano ukiwa ni mwaliko wa kanisa la Wasabato Libala la jijini Lusaka ambapo kwaya hiyo itashiriki katika maonyesho makubwa matatu nchini humo yanayotarajiwa kuanza siku ya jumamosi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kundi hilo matamasha hayo ambayo yatakuwa na viingilio ili kusaidia ujenzi na huduma ya kanisa la Libala yatafanyika katika ukumbi wa Blessing centre kisha uwanja wa mpira wa Levy Mwanawasa uliopo Ndola na kumalizia katika ukumbi wa New Government complex siku ya tarehe 2. Kwaya hiyo ambayo ilipata umaarufu sana nchini Tanzania mwaka 2011 kutokana na album yao ya Kwetu pazuri, imekuwa ikipata mialiko katika nchi mbalimbali za Afrika ambako wameonyesha kiu ya kuwaona waimbaji hao.

Ambapo kwa mwaka huu Ambassadors walishiriki tamasha la pasaka nchini Tanzania, tamasha ambalo hata hivyo liliwaweka katika wakati mgumu na makanisa ya kisabato nchini kutokana na kukubali kushiriki tamasha hilo, lakini pia walikuwa nchini Uganda pamoja na Goma nchini Kongo ambako wameshiriki katika matamasha mbalimbali ya kusaidia huduma za makanisa ya Kisabato.

Uwanja wa Levy Mwanawasa ulipo Ndola nchini Zambia,ambapo Ambassadors of Christ wataimba siku ya jumapili.

Habari na Gospel kitaa blog
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment