Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, November 29, 2013

KWA TAARIFA YAKO : JE WAJUA KWANINI JACKSON BENTY ANAJIITA MTAKATIFU?

Haya msomaji wetu wa Gospel Kitaa karibu katika kipengele chetu maalumu ''KWA TAARIFA YAKO'' ambacho kinakujia kila siku za alhamisi ndani ya GK kikiwa na lengo la kukupatia habari ambayo iliwahi kutukia lakini yawezekana huijui pia yawezekana ilitukia ukawa unaijua lakini GK ikawa imesahau mahali au kuna sehemu haina usahihi utapata fursa ya kusahihisha kwa kuweka comment yako chini kabisa kwenye habari husika. Karibu

Jackson Benty akiimba katika mkutano wa Injili wa Ufufuo jijini Arusha hivi karibuni.
KWA TAARIFA YAKO leo hii ni kuhusu mwimbaji nyota wa injili nchini anayeitwa Jackson Benty kutoka jijini Arusha, ni mwimbaji ambaye amekuwepo kwa muda mrefu sasa katika tasnia ya kueneza neno la Mungu kwa njia ya uimbaji na amefanyika baraka kwa watu wengi wanaosikiliza nyimbo zake.KWA TAARIFA YAKO je unajua mwimbaji huyu kwasasa anamtumikia Mungu katika kanisa la Ufufuo na Uzima la mchungaji Josephat Gwajima jijini Arusha?

Jackson ambaye amekuwa akipata mialiko ya kihuduma katika kanisa hilo hasa makao makuu yake Kawe jijini Dar es salaam, alianza rasmi ndani ya kanisa hilo mara baada ya kumalizika kwa mkutano wa injili ulioandaliwa na kanisa hilo huko jijini Arusha.KWA TAARIFA YAKO kama ilivyo makanisa mengi yanavyojipangia utaratibu wao ndivyo ilivyo kwa kanisa la Ufufuo na Uzima ambao mafundisho ya neno la Mungu ni kipaumbele cha kwanza unapojiunga, ambapo waumini wake wako katika madaraja mbalimbali ya utumishi kuanzia cheo cha potential shepherd cheo cha chini kabisa ambacho ndio ameanza nacho mwimbaji huyo.

Jackson Benty akimsifu Mungu katika kanisa la Ufufuo Arusha.
KWA TAARIFA YAKO Benty ana nyimbo nyingi zinazopendwa na watu kama uninyanyue, saa sita mchana, Ndiwe Mungu, Nipe raha na nyingine nyingi lakini pia ukiangalia katika baadhi ya makasha ya album zake Jackson amejiita St.Jackson Benty akimaanisaha Mtakatifu Jackson Benty alipoulizwa imekuwaje kujiita hivyo, Jackson amesema Mungu anapendezwa na watakatifu waliopo duniani ambao kat yao naye ni mmoja wapo. KWA TAARIFA YAKO Jackson Benty anajiandaa kutoa album mpya ikimpendeza Mungu hivi karibuni.

Habari na Gospel kitaa blog
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment