Writen by
sadataley
11:37 AM
-
0
Comments
Bajeti haina unafuu kwa walalahoi, wasema wananchi

Waziri wa Fedha, Dk William Mgimwa akiingia bungeni Dodoma jana kusoma hotuba ya Bajeti. Picha na Fidelis Felix.
Na Burhani Yakub,, Mwananchi
Tanga. Bajeti ya Serikali ilyosomwa Alhamisi iliyopita na Waziri wa Fedha, Dk William Mgimwa imezidi kukosolewa kwamba inalenga katika kuwanyonya wananchi wa kipato kidogo na kuwanufaisha vigogo.
Mkurugenzi Mtendaji wa asasi isiyo ya kiserikali inayojihusisha na Utawala Bora ya jijini Tanga, Ashery Vurugu, alisema ni bajeti isiyokuwa na huruma kwa walalahoi.
Alisema Serikali imeweka msamaha wa kodi ya pikipiki za bodaboda, lakini wakati huohuo imepandisha bei ya petroli, jambo ambalo alisema ni kuwaumiza wananchi.
“Leseni ya barabara ni mara moja tu kwa mwaka, lakini mafuta ni kila siku sasa Serikali inapopandisha bei ya mafuta na kusema imewawekea mazingira mazuri watu wa pikipiki inamaanisha nini,”alisema Vurugu.
Alisema bajeti ya Serikali ya mwaka 2013/14 ni ya kuwanyamazisha midomo wabunge ili wasizungumzie kasoro zake, lakini ifahamike kwamba ni wawakilishi wa wananchi ambao kupandishiwa bei ya mafuta ni kuwakamua hata kile kidogo walichonancho.
Aliwataka wabunge watakapoanza kuichambua bungeni, kuhakikisha kuwa mianya ya ukwepaji kodi kwa wafanyabiashara wakubwa na wawekezaji, inazibwa.
Bajeti hiyo iliyosomwa sambamba na bajeti za serikali zingine za nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, imelalamikiwa na wananchi wakidai kuwa hailengi katika kuwapa unafuu wa maisha. Wanalalamikia bei ya petroli.
No comments
Post a Comment