Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Sunday, March 11, 2018

Urusi yafanyia majaribio kombora lisiloweza kuzuiwa

missile with streak of light behind it

Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionKombora la Kinzhal linaelezwa kuwa linaweza kusafiri mara kumi ya kasi ya sauti na linaweza kufika hadi kilomita 2,000
Urusi inasema kuwa imefanakiwa kulifanyia majaribio kombora lake lisiloweza kuzuiwa, moja ya makombora yaliyotangawa na Rais Vladimir Putin mapema mwezi huu.
Ilisema 'lengo' la kombora hilo liligongwa.
Tarehe mosi mwezi huu , Rai Putin alitangaza kuwa kombora la Kinzhal na la kiwango cha juu.
Kombora la Kinzhal linaelezewa kuwa linaweza kusafiri mara kumi ya kasi ya sauti na linaweza kufika hadi kilomita 2,000.
Wizara ya ulinzi ilisema kuwa kombora hilo lilifyatuliwa kutoka kwa ndege aina ya MiG-31 ambayo ilipaa kutoka uwanja ulio kusini magharibi mwa Urusi siku ya Jumamosi.
"Uzinduzi huo ulienda kulingana na mpango, kombora hilo liligonga lengo lake," wizara ilisema.
Putin anatarajiwa kuchaguliwa tena kama rais wa Urusi wiki moja inayokuja.
Kama sehemu ya hotuba yake kwa taifa ya tarehe mosi mwezi hu, alicheza kanda ya video ambayo ilionekana kuonyesha mvua wa makombora katika jimbo la Florida nchini Marekani.
Marekani ilijibu ikisema kwa hiyo haistahili kuwa taibia ya taifa kama Urusi.

BBC

« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment