UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

Thursday, March 15, 2018

Serikali ya Afrika Kusini yatangaza rasmi ukame kama janga la taifa


Serikali ya Afrika kusini imetangaza rasmi ukame na uhaba wa chakula kama majanga ya taifa hilo.

Kwa mujibu wa taarifa waziri Zweli Mkhize amesema kuwa janga hilo limekumba maeneo matatu kati ya tisa Afrika Kusini.

Cape  Town, mji muhimu katika masuala ya utalii ni kati ya maeneo yaliyoathiriwa na ukame.

Miji mingine iliyokumbwa na janga hilo ni Northern Cape, Eastern Cape, na the Western Cape.

Afrika Kusini imekuwa ikipata mvua kidogo au mvua kutonyesha kabisa kwa miezi kadhaa kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa.

Mabwawa wengi nchini yamepungua kiwango cha maji .

Waziri Mkhize amesema kuwa ni takriban bilioni 6 zilitengwa katika bajeti ya mwaka 2017-2018 kusaidia kupambana na janga hilo.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment