Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, July 22, 2017

ACP Mwakalukwa: Kibiti shwari, anayetaka na aende

Dar es Salaam. Msemaji wa Jeshi la Polisi, kamishina msaidizi wa Polisi (ACP), Barnabas Mwakalukwa, amesema hali ya usalama katika wilaya za Mkuranga, Kibiti na Rufiji imeimarika sana na watanzania wanaweza kwendsa huko kufanya shughuli zao buila woga.

Ameyasema haya wakati akizungumza na wahariri wa Mwananchi Communications Limited (MCL) alipofanya ziara ya kujionea shughuli za kampuni hiyo.

ACP Mwakalukwa amesema tangu kuanzishwa kwa kanda maalum ya polisi katika eneo hilo, matukio ya uhalifu yamepungua na polisi wameweza kwa kiasi kikubwa kuwadhibiti watu waliokuwa wanafanya uhalifu.

Hata hivyo, ameviomba vyombo vya habari na waandishi nchini kusaidia kusambaza taarifa hizo ili kurudisha Imani ya wananchi.

“Zile taarifa kuwa sasa hivi eka 3,000 za ardhi Kibiti zinauzwa sh1,000 na hakuna mtu anayekwenda si za kweli. Hivi sasa hali ni shwaari Kibiti ana anayetaka kwenda anede… hata mimi nitakwenda huko,” amesema na kuongezaa:

“Mimi Nina mpngo wa kwenda kibiti bila vyombo vya habari… Andikeni habari nzuri za Kibiti, Hata nikitoka Leo muandike Kibiti shwari.”
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment