Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, July 22, 2017

Wizara ya Madini yafanya mabadiliko haya

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Mdoe (kulia).
mwaka 2010.

Wizara ya Nishati na Madini imefanya mabadiliko ya Sheria ya Madini kwa kuongeza malipo ya mrabaha kutoka asilimia 4 hadi 6 kwa madini ya Metali (dhahabu, shaba na fedha) ambapo mabadiliko hayo yametokana na marekebisho ya sheria ya madini ya

Hayo yamebainishwa na Kaimu Katibu Mkuu Prof. James Mdoe alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam kuhusu mabadiliko hayo na kusema kila anayetaka kusafirisha madini lazima yakaguliwe pamoja na kuthaminishwa kabla kuondoka katika ardhi ya Tanzania.

"Kupitia marekebisho ya sheria za fedha na sheria ya kodi, hivi sasa kila mtu au kampuni anayetaka kusafirisha madini nje yatakaguliwa na kuthaminishwa na atalipa ada ya ukaguzi ambayo ni asilimia 1 ya thamani ya madini anayosafirisha. Pia mchimbaji mdogo anayeuza madini kwa 'Broker au kwa 'Dealer' atakatwa asilimia 5 ya thamani ya madini kama 'with holding tax' ambayo itakusanywa na 'Broker' au 'Dealer' na kupelekwa TRA",amesema Prof. Mdoe.

Pamoja na hayo, Prof. Mdoe amesema katika kipindi hiki cha mpito serikali imesimamisha utoaji wa leseni za utafutaji na uchimbaji wa madini mpaka pale Tume itakapoundwa na kuanza kazi yake rasmi japokuwa kwa sasa shughuli zote zitafanyika chini ya usimamizi wa Kamishna wa Madini.

Kwa upande mwingine, Prof. Mdoe amesema kufutwa kwa TMAA na ofisi za madini za kanda, watumishi waliyokuwa wanafanya kazi kwenye Taasisi au Ofisi hizo ambao hawana tuhuma zozote wataendelea na ajira zao kama kawaida kwa sababu ni watumishi wa serikali katika Wizara ya Nishati na Madini.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment