Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, November 1, 2014

Kukatika kwa umeme Bangladesh gizani

   
Njia ya umeme wa msongo mkubwa Bangladesh
Bangladesh imekumbwa na tatizo kubwa la ukosefu wa umeme baada ya njia ya umeme inayounganisha nchi hiyo na umeme wa gridi ya taifa kutoka India kukatika.
Kukatika kwa umeme kulianza saa za mchana kwa saa za Bangladesh na kuathiri maeneo yote ya nchi hiyo yanayounganishwa na umeme wa gridi ya taifa.
Maafisa wamesema wahandisi wanafanyakazi ya kurekebisha tatizo hilo, ambalo chanzo chake bado hakijafahamika.
Ramani ya Bangladesh
Bangladesh ilianza kununua umeme kutoka India mwezi Oktoba mwaka jana.
Mkuu wa umeme wa gridi ya taifa nchini Bangladesh, Chowdhury Alamgir Hossain, ameliambia gazeti la Dhaka Tribune kwamba kukatika kwa umeme kulianza baada ya kutokea hitilafu katika kituo kidogo cha kusambaza uememe unaotoka India.
Hali hiyo ilisababisha mitambo mingine ya umeme nchini Bangladesh kuzimika mmoja baada ya mwingine, amesema Bwana Hossain.
Maafisa kutoka Bodi ya Maendeleo ya Umeme wameliambia gazeti la Daily Star nchini Bangladesh kuwa wanatarajia kurejesha hali ya kawaida ya umeme ifikapo saa tisa alasiri kwa saa za huko.
Njia ya umeme mkubwa inatoka Baharampur Bengal Magharibi kwenda Bheramara katika wilaya ya Kushtia, kusini magharibi mwa Bangladesh.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment