Writen by
sadataley
5:12 PM
-
0
Comments
Chaguo la GK siku ya leo ni kutoka kwa mwanamama Upendo Nkone ambaye ni mke wa askofu Mbeyela, wimbo tuliokuchagulia kutoka kwake ni ule uliotamba na kuendelea kuwepo masikioni mwa watu mpaka leo hii 'Usifurahi Juu Yangu'. Wimbo huu umerekodiwa jumapili iliyopita wakati mwanamama huyu akiimba katika viwanja vya Tanganyika Packers Kawe jijini Dar es salaam kwenye ibada ya shukurani kwa Mungu iliyoandaliwa na kanisa la Ufufuo na Uzima.
Nimatumaini yetu kwamba utabarikiwa kupitia wimbo huu kwamba licha ya kuimbwa kwa cd lakini utaona mwimbaji na waumini walivyouimba kwa kumaanisha na kuonyesha uwepo wa Mungu ulivyofunika eneo hilo. Barikiwa
![]() | |
Upendo na mumewe Askofu Mbeyela. Habari na Gospel kitaa |
No comments
Post a Comment