Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, May 17, 2014

Ukawa: CCM haiwezi kuleta Katiba Mpya


Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Taifa wa Chadema, John Heche 
Na Waandishi Wetu, MwananchiDodoma. Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) nje ya Bunge umesema hatima ya kupata Katiba Mpya utaamuliwa na wananchi na wala siyo chama tawala.
Kauli hiyo inatolewa ikiwa ni siku moja baada ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uratibu na Uhusiano), Stephen Wassira kusema Ukawa wasiporejea bungeni, kanuni zitabadilishwa na Bunge litaendelea.
Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Taifa wa Chadema, John Heche alisema hakuna nchi inayoandika Katiba kwa kushirikisha kundi moja.
Alisema Ukawa hawatarejea bungeni pamoja na vitisho vinavyotolewa na viongozi mbalimbali wa Serikali ya CCM hadi pale mjadala wa kuijadili Rasimu ya Mabadiliko ya Katiba utakapozingatiwa.
“Acha wajidanganye kubadili kanuni, lakini mwisho wa siku wananchi wanajua kinachofanywa na CCM, hatima ya Katiba Mpya iko mikononi mwao,’ alisema Heche na kuongeza:
“CCM haina nia ya kupata Katiba Mpya, kwani viongozi wake wamekuwa wakisema Katiba iliyopo inafaa, jambo ambalo tunashindwa kuelewa kwa nini imetoa mabilioni kuratibu mchakato huu.”
Katika hatua nyingine, Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania imejiunga na Ukawa unaoundwa na vyama vya Chadema, NCCR-Mageuzi na CUF katika mikutano inayoendelea nchi nzima.
Msemaji wa Jumuiya hiyo, Sheikh Rajabu Katimbo alisema malengo mazuri ya Ukawa ndiyo yaliyowashawishi kujiunga.
Alisema taasisi zake zimeunga mkono harakati za Ukawa kutokana kwa vile CCM imedhamiria kutupa kutupa maoni ya wananchi kupitia Rasimu ya pili ya Katiba iliyowasilishwa bungeni na Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba.
Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika juzi katika Viwanja vya Mwembetogwa mjini hapa, Katimbo alisema kilichofanywa na Wajumbe wa Bunge la Katiba kutoka CCM ni ukiukwaji wa haki kwa wananchi.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment