Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, May 17, 2014

Watu 10 wafa katika mlipuko wa bomu


Polisi wakijitahidi kudhibiti umati wa watu waliofika kushuhudia eneo lililotokea mlipuko wa Guruneti nje kidogo ya jiji la Nairobi nchini Kenya jana.Takribani watu 10 wanahofiwa kufariki na 70 kujeruhiwa.Picha na Tony Karumba 
Na Na Mwandishi Wetu
Nairobi. Watu 10 wamefariki dunia na wengine zaidi ya 70 kujeruhiwa baada milipuko miwili kutokea karibu na soko kubwa la nguo la Gikomba mjini Nairobi.
Kuna uwezekano idadi hiyo ya watu waliofariki dunia ikaongezeka kutokana na hali ya baadhi ya majeruhi kuwa mbaya.
Milipuko hiyo imetokea siku moja baada ya nchi za magharibi ikiwamo Uingereza kuwataka raia wake wanaoishi nchini humo kurejea nyumbani kwa hofu ya usalama.
Jeshi la polisi limesema kuwa linamshikilia mtu mmoja kwa madai ya kuhusika kwenye tukio hilo na hakuna taarifa zaidi zilizotolewa.
Msemaji wa Hospitali ya Kenyatta aliliambia Shirika la Habari la AFP kuwa baadhi ya majeruhi waliopelekwa hospitalini hapo hali zao ni mbaya.
Mfanyabiashara mmoja aliyekuwepo kwenye eneo la tukio alisema kuwa alisikia mlio mkubwa uliofuatiwa na moshi uliotanda eneo lote la soko na kwamba baada ya tukio hilo watu wengi walikimbia ovyo kuokoa maisha yao.
“Watu wengi wamejeruhiwa. Sijui idadi ya watu waliopoteza maisha, lakini kusema kweli mlipuko huu ni mkubwa na utakuwa umeleta madhara makubwa,” alisema Mwangi Maina.
Hadi sasa hakuna kundi lililodai kuhusika na tukio hilo, lakini wachunguzi wa mambo wanalitaja Kundi la Al-Shabaab kuwa huenda likawa nyuma ya matukio hayo.
Kenya imekuwa ikiandamwa na matukio ya kigaidi tangu ilipopeleka askari wake nchini Somalia kukabiliana na kundi lenye msimamo mkali wa Kiislamu, Al-Shabaab.
Taarifa zilizotolewa na vyombo vya habari vya nchi za magharibi zinasema kuwa zaidi ya watu 100 wamepoteza maisha katika kipindi cha miezi 18 iliyopita tangu Kenya ianze kuandamwa na mashambulizi ya kigaidi.
Milipuko hiyo imekuja huku raia wengi wa kigeni waliokuwa nchini Kenya kwa shughuli za utalii wakiwa wanarejea nyumbani kuitika wito uliotolewa na serikali zao.
Tahadhari hiyo kutoka kwa Serikali ya Uingereza ilieleza kuwa askari wa Al-Shabaab, huenda wakafanya mashambulizi nchini Kenya katika muda wowote kuanzia sasa.
Kwa habari zaidi ingia http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Watu-10-wafa-katika-mlipuko-wa-bomu/-/1597296/2318040/-/1s09ntz/-/index.html
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment