Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Sunday, August 4, 2013

WANAJESHI ZAIDI WAHITAJIKA SOMALIA

Uganda imetoa wito wanajeshi zaidi wa Afrika wapelekwe katika kikosi kilioko Somalia, ili kikosi hicho kiweze kujizatiti katika maeneo iliyoyakomboa kutoka wapiganaji wa Kiislamu, Al Shabaab.
Maafisa wa kikosi cha AMISOM, Somalia
Waziri wa Mashauri ya Nchi za Nje wa Uganda, Sam Kutesa, alisema kati ya wanajeshi 2,000 hadi 20,000 zaidi wanafaa kupelekwa Somalia.
Viongozi wa nchi zilizochangia wanajeshi wanakutana na rais wa Somalia mjini Kampala, Uganda.
Msemaji wa rais wa Somalia, Abdirahman Omar Osman, alieleza kuwa kikosi cha kimataifa kitawekwa katika mji muhimu wa Kismayo.
Somalia imewashutumu wanajeshi wa Kenya walioko Kismayo kwamba wana msimamo wa upendeleo.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment