Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Sunday, August 4, 2013

ZUMA AMPA HONGERA KUBWA MUGABE

Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini ametoa zile alizoita, hongera nyingi kwa Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe, ambaye ameshinda muhula wa saba wa uongozi akiwa na umri wa miaka 89.
Zuma akikaribishwa na Mugabe alipozuru Harare zamani
Rais Zuma amesema uchaguzi mkuu wa Zimbabwe ulifanikiwa, na ametoa wito kwa pande zote zikubali matokeo.
Mpinzani mkuu wa Bwana Mugabe, Morgan Tsvangirai, mwenye umri wa miaka 61, amekataa matokeo na amesema atapeleka malalamiko mahakamani.
Viongozi wa mataifa ya magharibi yamesema yana wasi-wasi kama uchaguzi ulikuwa wa halali.
Bwana Mugabe alipata asili-mia-61 ya kura katika uchaguzi wa rais.
Na chama chake cha ZANU-PF kilipata thuluthi mbili ya viti vya bunge.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment