Writen by
sadataley
9:03 PM
-
0
Comments
Ibrahim Boubacar keita
Mgomboea urais nchini Mali Soumalia Cisse amekubali kushindwa na mpinzani wake Ibrahim Boubacar Keita katika duru ya pili ya uchaguzi uliofanyika Jumapili. Akizungumza Jumatatu jioni Cisse alisema bw. Keita alishinda uchaguzi huo kwa njia halali na kumtakia kila la kheri.
Msemaji wa bw.Keita, Mamadou Camara alisema matokeo yanaonyesha kuwa alipata kati ya asili mia 70 na 80 ya kura.Camara alisema bw. Cisse alimtembelea Keita nyumbani kwake Jumatatu jioni na kumpongeza kufuatia ushindi huo.
Akizungumza na idhaa ya Kifaransa ya Sauti ya Amerika Jumanne msemaji huyo alisema kuwa ushindi wa bw. Keita ulikuwa mkubwa na kwamba sasa ataelekeza nguvu zake zote katika kuleta maridhiano ya kitaifa nchini Mali.
Imewkwa na Happy Adam
No comments
Post a Comment