Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, August 3, 2013

KKKT DAYOSISI YA IRINGA USHARIKA WA KANISA KUU WAFANYA KONGAMANO LA VIJANA KATIKA CHUO KIKUU IRINGA

KANISA LA KIINJILI LA KILUTHERI TANZANIA 


DAYOSISI YA IRINGA 

NAFASI YA KIJANA KATIKA KANISA.

SOMO LILOTOLEWA KATIKA KONGAMANO LA VIJANA  KATIKA USHARIKA  WA KIHESA 29-06-2013

  1. KANISA NI NINI?
    Kanisa  si jengo  tu bali ni wale waliomo ndani yake. Maana yake ya asili toka neno la Kiyunani ni ekklesia “kusanyiko” walioitwa kama maneno katika msalaba ambao huwa ninauvaa. Neno Kanisa Iimo katika Biblia, Matendo ya mitume 17:24 "Mungu aliyeufanya ulimwengu na vitu vyote vilivyomo yeye kwa kuwa ni Bwana wa mbingu na nchi, hakai katika hekalu zilizojengwa kwa mikono."
Kanisa ni watu wanao amini Waefeso 2:21 "Katika yeye jengo lote linaungamanishwa vema na kukua hata liwe hekalu takatifu katika bwana." 1Wakorintho 3:16 "Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu na yakuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?.
Kazi ya kanisa ni ipi? Kanisa linaeneza ijili  2 Timotheo 4:2 "Lihubiri neno uwe tayari wakati ufaao na wakati usiokufaa karipia kemea na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho."
Kanisa limepewa maagizo na Mungu Waefeso 4:12 "Kwa kusudi kuwakamilisha watakatifu hata kazi ya huduma itendeke hata mwili wa Kristo ujengwe."
Kila mshiriki ana jukumu maalum 1 Wakorintho 12:13, "Kwa maana katika Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja kwamba tu wayahudi au kwamba tu wayunani ikawa tu watumwa au ukawa tu huru nasi tulinyweshwa Roho mmoja."
Wakristo tu wafariji wenzetu Waebrania 10:25 "Wala tusiache kukusanyika pamoja kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane na kuzidi kufanya hivyo kwa kadiri muonavyo siku ile kuwa inakaribia.
B. KIJANA  NANI
1.     Ujana ni hatua ambayo mtu anaipitia baada ya utoto au ni kipindi cha kati cha makuzi ya mtu kabla ya utu uzima na hatimae uzee
2.    Ujana huanza mara baada ya mtu kubadilika kimaubile na huanzia miaka kumi na mbili wengine hadi kumi na tano ambapo mtu huanza kuwa na hisia za kimwili na kutamani sana kuwa na uhuru wake katika maamuzi. Mabadiliko haya huchochea au hupelekea hisia mbalimbali za kimwili na mabadiliko ya jumla ya tabia
3.    Ujana ni majira yanayopita katika makuzi ya mwanadu, ukifanikiwa kuwa mzee ni lazima ulipita katika kipindi hiki au daraja hili la ujana, kwa hiyo kama bado uko katika dara hili ni muhimu kujipanga ili usije ukajilaumu mbele ya safari
UMRI WA KIJANA KIKANISA
Kanisa linamtambua kijana baada ya kupata kipaimara wengi hupata kuanzia miaka kumi na miwil-kumi nan ne na ukomo wa ujana ni miaka arobaini na tano (12-45)
Hivyo napenda kusema kuwa ndiyo sababu siku zote nikijitazama kama kijana humuona Mungu kuwa ni wa ajabu kuniumba hata mimi na kunifanya kuwa Mchungaji. Hivyo hukubaliana na nyimbo na waimbaji hawa ambao wamewahi sema kupitia nyimbo zao kuwa

a.            “Mungu wetu ndiye Boma”- Tumwabudu Mungu Wetu 302 na Dr. Martin Luther
Mungu ndiye ngao yetu na siraha yetu shetani akija kwetu tukiwa naye daima tutashinda na maadui zetu (shida,adha na changamoto za maisha yetu  yote). Tumtazame yeye kama Dr. Martin Luther alivyosema katika maneno ya wimbo wake huu. Anaimba wakati akiwa katikati ya mapambano na sisi tuimbe tunapopita katika hali mbalimbali katika maisha yetu.
b.            “Mungu ni Mwaminifu”. -Solomon Mkubwa
Mungu hatotuacha daima yeye hutunza maagano(makubaliano yetu nay eye) hivyo hata sisi tulivyo hapa anatujua na anaendelea kutunza uaminifu wake kwetu hivyo na sisi tusimame kwake tu, tumtazame yeye pekee.

c.            “Liseme kwani ni jambo usilolijua”- Sarah K
 kwani ni hakika hatuna tunalolijua katika maisha yetu ni yeye (Yesu) anatuwezesha ,ametuwezesha na ataendelea kutuwezesha.

d.            “I will be There, Just Call My name”. -Michael Jackson&Mariah Carey
Ipo siku tutaitwa kwenda Mbinguni na kila mmoja wetu ataitwa kwa jina lake; hivyo tujiandae.

e.            “Heri Kumjua Yesu Bwana”.  Tumwabudu Mungu Wetu 175 na F.J Crosby
Ni Yesu pekee atatuwezesha na kutuvusha na hata sasa anajua tulikotoka,tulipo na tuendako.

f.             “Msingi wa Kanisa Ndiye Yesu Bwana”. Tumwabudu Mungu Wetu 268 na samuel Stone
Kama tulivyoimba siku ile ya Kipaimara hebu tuendele kumtazama yesu kama msingi wa Kanisa na ndiyo njia pekee ya kutuvusha vijana, njooni tumtumikie kadili ya nafasi tunazojali. Tusiogope huku ni kuzuri tu hakuna shida yoyote.

KIJANA KAMA
  1. MSHARIKA MKAMILIFU ALIYEPO NA AJAYE

  1. KIONGOZI WA KANISA-MZEE WA KANISA-MTUMISHI WA MUNGU KATIKA KADA MBALIMBALI


  1. MLEZI WA FAMILIA   AJAYE NA ALIYEPO (wajibu wako pale nyumbani kwa sasa).
  2. MZAZI AJAYE – (unayoyafanya sasa nawe utafanyiwa na m/watoto wako).
  3. MTETEZI WA WANYONGE (Haki za wanyonge na wanaonyanyaswa kuto kaa kimya kwani Dr. Martin Luther alisema utawajibika kwa yale uliyoyasema na usiyoyasema lakini ulipaswa kuyasema na umekaa kimya.)

  1. MWANA MAENDELEO ( Jiandae kuajili au kuleta mabadiliko katika eneo ambalo Mungu atakupa/amekupa).

A.    “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako kabla hazijaja siku zilizo mbaya…” (Mhubiri12:1)

B.    “Nimewaandikia ninyi vijana, kwa sababu mna nguvu, na neno la Mungu  linakaa ndani  yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu”.
             (I Yohana 2:14b).

C.   “Na nimwibie mpenzi wangu wimbo wa mpenzi wangu katika habari za shamba lake la mzabibu. Mpenzi wangu alikuwa na shamba la mizabibu,kilimani penye kuzaa sana;akafanya handaki kulizunguka pande zote, akatwaa mawe yake,akapanda ndani yake mzabibu ulio mzuri, akajenga mnara katikati yake, akachimba shinikizo ndani yake;akatumaini ya kuwa utazaa zabibu, nao ukazaa zabibu-mwitu. Na sasa, enyi wenyeji wa yerusalem, namyi watu wa Yuda amueni, nawasihi mkato, kati ya mimi na shamba  langu la mizabibu….”(Isaya 5:1-7). 

MAMBO YA KUZINGATIA NI:-
“Huwezi kuyajali maisha yako kama hujui thamani yake, huwezi kujua thamani ya maisha yako kama hujajitambua kwa Neno la Mungu, huwezi kuwa na maisha ya mafanikio kama maamuzi yako hayatengenezi mafanikio, ufahamu sahihi juu ya maisha yako ndio msingi wa kujitambua kwako, yaani kuijua Kweli ili hiyo Kweli ikuweke huru na ndipo utakapokuwa huru kweli kweli, kumbuka hata usipoamua maisha yako yataendelea kama kawaida. Zaidi ya hayo kama hujui wewe ni nani huwezi kujua thamani yako, kama hujui thamani yako lazima utaishi chini ya kiwango cha maisha unayotakiwa kuishi”.
UTAIJUAJE NAFASI YAKO KAMA KIJANA
Nafasi yako kama Kijana ni wajibu wako, umuhimu ulionao kwako na kwa jamii kwa ujumla wake pamoja na familia yako. Lazima ujue nafasi yako katika maeneo yafuatayo:
• Kwako binafsi,
• Katika familia yako,
• Kwa Kanisa lako,
• Kwa jamii yako
• kwa mkoa wako,
• kwa Taifa lako na
• kwa Ufalme wa Mungu.
Safari ya kujua nafasi yako katika maeneo yako hayo  hayo hapo juu  inaanzia katika eneo moja tu ambalo ni KUJITAMBUA
KUJITAMBUA NI NINI
“Kujitambua ni hali ya kuwa na ufahamu au uelewa (kujua) wa kutosha juu ya maisha yako kwa ujumla pamoja na mazingira yanayokuzunguka na hivyo kukufanya uishi maisha yanayofanana au kulingana na kusudi la Mungu kwako, uishi katika ubora wa maisha yanayolingana na kiwango cha ufahamu ulionao au kiwango cha kujitambua kwako kutegemeana na nguvu ya taarifa unazopata.
HIVYO BASI KIJANA ANATAKIWA  KUJUA KUWA:-
1. Kujitambua ni hatua ya muhimu katika maisha ya mtu yoyote duniani kama anataka kuishi kwa Furaha na matumaini na kufikia malengo yake
2. Kujitambua ni matokeo ya kupata ufahamu sahihi juu eneo fulani utakaokusaidia kufanya maamuzi sahihi katika eneo husika ili uweze kufanikiwa
3. Ufahamu au maarifa unapatikana kwa kutafuta, kuchunguza na kudadisi taarifa mbalimbali kwani si kila namna ya kujitambua ni sahihi kwa kijana
4. Matokeo ya ufahamu ulionao yatafanana na ubora wa maisha unayoishi kwa kiwango cha kuathiri maamuzi yako ya kila siku
5. Kiwango cha matokeo ya kujitambua kitafanana na ubora wa taarifa ulizozipata
6. Udhihirisho wa maisha ya kujitambau ni hatua ya juu kabisa ya kuthibitisha kwamba kweli umejitambua.
KWANINI KUJITAMBUA NI LAZIMA:-
1. Ni lazima ujitambue, upate ufahamu sahihi juu ya maisha yako pamoja na mambo yote na jamii inayokuzunguka
2. Ni muhimu ujue wajibu ulionao kwako wewe mwenyewe kama mtu binafsi juu ya maisha yako
3. Kuna haja ya kujua kuwa wewe ni sehemu ya familia yako na lazima ujue wajibu wako kwa wazazi na familia kwa ujumla
4. Ni lazima ujifunze kuwa mzalendo wa taifa lako sawa na jinsi ambavyo Mungu anataka, fahamu kuwa umeunganishwa na ardhi ya Tanzania kwa mafanikio yako, Mungu akikwambia nenda nje ya nchi nenda lakini usifikiri mafanikio hayako Tanzania
5. Kijana anatakiwa ajitambue, ajielewe yeye ni nani na ana kusudi gani katika maisha yake
6. Unatakiwa kupata uelewa wa kutosha juu ya kipindi cha ujana na umuhimu wake ukiwa bado Kijana ili ujue namna ya kuzingatia na kujipanga kwa hapo baadae
7. Kuelewa changamoto zilizopo katika kipindi cha ujana na namna ya kuzishinda kuna uhusiano na namna unavyojitambua ukiwa bado kijana
8. Kujenga shauku, nia na kiu kwa kijana ili aweze kuishi maisha yenye mwelekeo na aweze kutimiza maono yake akiwasaidia na wengine kumjua Mungu na maisha yake kwa ujumla wake
9. Kuwekeza uthamani na nguvu ya kipindi cha ujana kwa mtazamo wa Ufalme wa Mungu.
KIJANA MWENZANGU CHUKUA MUDA KUTAFAKARI MISTARI HII
Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. - Yohana 3:16
kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu; - Warumi 3:23
Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu. - Warumi 6:23
Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi. - Yohana 14:6
Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake; - Yohana 1:12
Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu. - Yohana 3:3
Na katika Torati karibu vitu vyote husafishwa kwa damu, na pasipo kumwaga damu hakuna ondoleo. - Waebrania 9:22
akasema, Amin, nawaambia, Msipoongoka na kuwa kama vitoto, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni. - Mathayo 18:3
Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami. - Ufunuo wa Yohana 3:20
Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote. - I Yohana 1:9
Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka. Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu. kwa kuwa, Kila atakayeliitia Jina la Bwana ataokoka. - Warumi 10:9,10,13
Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu; wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu. - Waefeso 2:8,9
si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyoyatenda sisi; bali kwa rehema yake, kwa kuoshwa kwa kuzaliwa kwa pili na kufanywa upya na Roho Mtakatifu; - Tito 3:5
Wakamwambia, Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka pamoja na nyumba yako. - Matendo ya Mitume 16:31
Amwaminiye Mwana yuna uzima wa milele; asiyemwamini Mwana hataona uzima, bali ghadhabu ya Mungu inamkalia. Yohana 3:36
Nami nawapa uzima wa milele; wala hawatapotea kamwe; wala hakuna mtu atakayewapokonya katika mkono wangu. - Yohana 10:28
Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya. - II Wakorintho 5:17
Imeandaliwa na
Mchg Kurwa Sadataley- Mratibu wa Idara

 Habari na Mawasiliano KKKT-DIRA
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment