Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, February 29, 2020

Faida ya Embe bichi kiafya


Unaweza usiamini nikikuambia embe bichi ni tiba ya ugonjwa furani, lakini amini kuwa kweli ni tiba, tena iliyo makini. Embe bichi linasaidia sana kwa mgonjwa wa maradhi ya kuhara. Tumia embe bichi kumaliza tatizo hilo.

Menya embe bichi, likate  vipande na kuviweka katika chombo, au tengeneza juice changanya na unga wa pilipili manga pamoja na asali, kisha tafuna vipande hivyo vyenye mchanganyiko huo.

Mchanganyiko wako utategemea kiwango cha vipande vya embe lako. Hata hivyo, usile zaidi ya embe mbili kwa kutwa moja. Endelea na tiba hii muda wa siku tatu.

Kuharisha ni kitendo cha kujisaidia kinyesi chenye majimaji mara kwa mara. Hali hiyo hutokea baada ya utumbo mdogo kuwa na maji mengi ambayo yanashindwa kutoka mwiilini kwa njia za kawaida kama ya mkojo na jasho hivyo yanatelemka kwenye utumbo mkubwa usio na uwezo wa kutunza maji.

Yakiwa huko mtu hujikuta anajisikia hali ya kutoa haja na ndipo maji hayo hutoka kupitia haja kubwa. Kimsingi utumbo mdogo una uwezo wa kupokea zaidi ya lita nane za maji kutoka kwenye vyakula au vinywaji vinavyopitia mdomoni na mengine kutoka sehemu mbalimbali katika mwili.

Tatizo la kuhara linaweza kusababishwa na kula kupita kiasi, kula mchanganyiko wa vyakula vya aina mbalimbali, kuwa na hofu, hasira au wasiwasi, kuchacha chakula ndani ya tumbo, kula sumu, bakteria, virusi au vijidudu wenye vimelea.

MUUNGWANA BLOG
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment