Mauritania yajiunga na mataifa ya Ghuba kwa kutangaza kusitisha ushirikiano wake wa kidiplomasia ya Qatar.
Mauritania imekuwa nchi ya 8 miongoni mwa mataifa yaliotangaza kusitisha ushirikiano wake na Qatar.
Taarifa ya Mauritania kusitisha ushirikiano wak e na Qatar ilitolewa kupitia kituo cha habari cha AMI.
Wizara ya mambo ya nje ya Mauritania imefahamisha katika tangazo lake kuwa serikali imechukua hatua hiyo ngumu kwa ajili ya kulinda maslahi ya kiarabu.
Saudia Arabia , Misri, Bahrein, UEA, Yemen, Libya na Maldives zilitangaza siku mbili zilizopita kusitisha ushirikiano wa kidiplomasia na Qatar.
Mauritania imejiunga na mataifa hayo kwa kutangaza pia kusitisha ushirikiano wake na Qatar.
Usafiri wa aina yeyote kutoka katika matifa hayo kuelekea Qatar umesitishwa.
Raia wa Qatar wamepewa siku 14 kuondaka Saudia Arabia.
Ikawa ushirikiano baina ya Qatar na Jordan ukiyumba, kituo cha habarşii cha al-Jazira kimefungwa nchini humo.
No comments
Post a Comment