Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Wednesday, November 2, 2016

Chuo kikuu cha Makerere chafungwa kutokana na mgomo.

Wahadhiri na wanafunzi wamekuwa kwenye mgomo

Image copyrightANDREW MOORE
Image captionWahadhiri na wanafunzi wamekuwa kwenye mgomo
Wanafunzi wameanza kuondoka kutoka Chuo Kikuu cha Makerere baada ya Rais Yoweri Museveni kutangaza kifungwe mara moja Jumanne jioni.
Rais alisema amechukua hatua hiyo "kuhakikisha usalama wa watu na mali."
Chuo kikuu hicho kilikuwa kimekumbwa na vurugu kutokana na mgomo wa wahadhiri na wanafunzi.
Chama cha wahadhiri Jumatatu kiliamua kuendelea na mgomo hadi wahadhiri walipwe marupurupu ya miezi minane ambayo yamefikia Sh32bn (dola 9.2 milioni za Marekani).
Wanafunzi walijiunga na mgomo Jumanne, na walitaka kukutana na Rais Museveni badala ya mwenyekiti wa baraza simamizi ya chuo chini ya uenyekiti wa Dkt Charles Wana-Etym.
Naibu chansela wa chuo hicho Prof Ddumba Ssentamu wiki iliyopita alikuwa amewasihi wahadhiri wakubali kurejea kazini huku suluhu ya kudumu ikiendelea kutafutwa.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment