Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, September 30, 2016

Rodrigo Duterte asema "anafurahia kuua" sawa na alivyofanya Hitler

Rodrigo Duterte akiwa Davao


Image copyrigh
Amesema anaweza kuua walanguzi wengi wa dawa hizo za kulevya sawa na alivyofanya Hitler akiua Wayahudi.
"Hitler aliua Wayahudi milioni tatu ... kuna waraibu milioni tatu wa dawa za kulevya. Ninaweza kufurahia sana kuwaua," amesema.
Wayahudi zaidi ya milioni sita waliuawa na Wanazi chini ya Hitler.
Bw Duterte amekuwa akiongoza kampeni kali ya kuua walanguzi na watu wanaotumia dawa za kulevya tangu achukue madaraka mwezi Juni.
Takwimu rasmi zinaonesha watu zaidi ya 3,000 wameuawa kwenye operesheni za polisi au na makundi ya kiraia.
Miili ya waliouawa huachwa hadharani, ikiwa na mabango yaliyoandikwa makosa waliotuhumiwa kutekeleza.
Rais huyo awali amesema anaweza kufurahia sana "kuua wahalifu 100,000" kupunguza viwango vya uhalifu Ufilipino.
'Maneno ya kukera'
Bw Duterte alikuwa akiongea Davao, mji ambao alikuwa meya zamani ambapo alitekeleza sera kali ya kuunga mkono makundi ya kuua wahalifu.


Manila, 21, Agosti 2016Image copyrig
Image captio

Ameambia wanahabari kwamba amekuwa akioneshwa na baadhi ya wakosoaji wake kama "binamu wa Hitler".
"Hitler aliua Wayahudi milioni tatu, kuna waraibu milioni tatu. Ninaweza kufurahia sana kuwaua," amesema.
"Angalau Ujerumani walikuwa na Hitler. Wafilipino hawawezi."


Rodrigo Duterte akibusu bendera Manila (7 Mei 2016)Image copyright

Amesema angependa sana "kumaliza tatizo hilo nchini mwangu na kuokoa vizazi vijavyo".
Matamshi yake yameshutumiwa na makundi ya Wayahudi, shirika la habari la Reuters limeripoti.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment