Latest News

GNM Cargo

GNM Cargo
GNM CARGO & LOGISTICS

menu

Saturday, July 2, 2016

Uganda yavunja mkataba na kampuni ya Urusi

Park Geun-hye alizuru Uganda mwezi Mei Serikali ya Uganda imevunja mkataba wake na kampuni ya Urusi kuhusu mpango wa kujenga kiwanda cha kusafisha mafuta. Serikali ilikuwa imekamilisha mazungumzo na kampuni hiyo ya Rostec Global Resources Consortium. Lakini inasema baadaye kampuni hiyo ilianza kuongeza masharti mengine hata baada ya makubaliano ya mwisho kufikiwa. Uganda kukata uhusiano na Korea Kaskazini Mkataba huo sasa umekabidhiwa kampuni ya SK Engineering kutoka Korea Kusini. Kampuni hiyo iliibuka ya pili katika shughuli ya kutoa zabuni. Hatua hiyo imejiri wiki chache baada ya Rais wa Korea Kusini Park Geun-hye kuzuru Uganda.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment