Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, April 15, 2016

Clinton na Sanders wajibizana vikali New York

Clinton amekuwa seneta New York naye Sanders ni mzaliwa wa jimbo hilo Wagombea urais waliosalia katika chama cha Democratic, Hillary Clinton na Bernie Sanders, wamejibizana vikali katika mdahalo uliofanyika katika jiji la New York. Kila mmoja ametilia shaka uwezo wa mpinzani wake kufanya uamuzi wa busara kuhusu masuala kama vile kudhibiti benki Wall Street, kudhibiti umiliki wa silaha na ujira wa chini. Jimbo la New York litafanya mchujo wake Jumanne. Bw Sanders amemkosoa Bi Clinton kwa kuunga mkono vita vya Iraq na kutetea mikataba ya biashara huru. Sanders amshinda bi Clinton huko Wyoming Lakini naye Bi Clinton amemtuhumu Bw Sanders na kusema hawezi kutekeleza hata sera zake mwenyewe, mfano kuvunja udhibiti wa benki kuu za Wall Street. Sanders ameshinda majimbo saba kati ya manane yaliyofanya mchujo karibuni Wote wawili wana uhusiano mkubwa na jimbo hilo la New York. Bw Sanders alizaliwa huko naye Bi Clinton amekuwa seneta wa jimbo hilo kwa miaka minane. Mdahalo huo wa runingani umefanyika eneo la Brooklyn. Bw Sanders ameshinda majimbo saba kati ya manane yaliyofanya mchujo karibuni jambo lililomuwezesha kupunguza uongozi wa Bi Clinton katika mchujo wa chama hicho. Clinton anajivunia uongozi mkubwa Bi Clinton hata hivyo bado anajivunia uongozi mkubwa. Uchaguzi mkuu nchini Marekani utafanyika mwezi Novemba.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment