Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Wednesday, March 25, 2015

Kinasa sauti cha ndege chaharibika

Waziri wa maswala ya ndani nchini Ufaransa, Bernard Cazeneuve, amesema kuwa kifaa cha kunasa sauti kwenye ndege kilichopatikana hapo jana Jumanne baada ya kuanguka kwa ile ndege ya Ujerumani katika milima ya Alps kimeharibika. Lakini Bwana Cazeneuve anasema kuwa kifaa hicho bado kitatoa taarifa kwa watalamu wanaojaribu kubaini kilicho sababisha kuanguka kwa ndege hiyo, ambayo iliwauwa abiria wote 150 na wahudumu waliokuwemo kwenye ndege hiyo. Shughuli za utafutaji wa ndege hiyo zimerejelewa baada ya usiku kumalizika. Ndege za helikopta zinaonekana zikipaa katika maeneo hayo huku maafisa wa polisi wakiendelea kuchunguza mabaki ya ndege . Maafisa wakuu wanaonya kuwa kupata mabaki ya miili ya abiria itachukua muda mrefu kutokana na hali mbaya ya anga katika eneo hilo. Ndege hiyo ilikuwa ikitoka Barcelona na kuelekea mji wa Duesseldorf. Kansela wa Ujerumani pamoja na Rais wa Uhispania na waziri wake mkuu, wanatarajiwa kuzuru eneo la ajali hiyo hii leo Jumatano.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment