Writen by 
                            sadataley
4:57 PM
                            - 
                            
0
                            Comments
                          

Wanaume wanaounga mkono mapenzi ya jinsia moja Uganda
Mahakama ya kikatiba nchini 
Uganda imefutilia mbali sheria dhidi ya wapenzi wa jinsia moja ambayo 
ilisababisha mataifa ya magharibi kuinyima msaada.
Kadhalika sheria hiyo ilizua gumzo sana sio tu 
Uganda bali kote duniani ambapo mataifa ya Magharibi yalilazimika 
kuingilia kati. Mahakama ilisema kuwa mswada huo kabla ya kuidhinishwa kuwa sheria ulipitishwa na wabunge ambao idadi yao haikutosha kupitisha mswada na kwa hivyo ni kinyume na sheria.

Baadhi ya waandamanaji waliounga mkono serikali kwa kuharamisha mapenzi ya jinsia moja
Mataifa kadhaa ya Magharibi yamesitisha msaada kwa Uganda hasa baada ya sheria hiyo mpya kupitishwa.
No comments
Post a Comment