Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, January 23, 2014

Shirikisho la Soka barani Afrika latenga kitita chadola kwa mshindi wa michuano ya CHAN

Rais wa Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF), Issa Hayatou
Rais wa Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF), Issa Hayatou

Na RFI
Shirikisho la soka barani Afrika CAF limetangaza kuwa mshindi wa michuano inayoendelea ya CHAN inayowahusisha wachezaji wanaocheza soka katika ligi za nyumbani atapata kitita cha DOLA 750,000.

CAF pia imesema kuwa Dola Milioni 3 nukta 2 ziltagawanywa miongoni mwa timu zote 16 zilizoshiriki katika kinyanganyiro hicho.
Haya yanajiri, huku Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Gabon zikijiunga na Mali, Nigeria, Morroco, Zimbabwe, Ghana na Libya katika hatua ya robo fainali.
Timu zote zilizokuwa zinawakilisha Afrika Mashariki zimeondolewa katika michuano hii, ikiwemo Uganda, Ethiopia na Burundi.
Katika michuano ya robo fainali zitakazopigwa mwishoni mwa juma hili, Morroco watapambana na Nigeria katika mchuano wa kwanza siku ya jumamosi, huku Mali wakimenyana na Zimbabwe.
Siku ya Jumapili, Gabon watamenyana na Libya, huku Ghana wakipangiwa kumaliza kazi na Jamhuri ya Kidemkorasia ya Congo.
Michuano ya robo fainali itachezwa siku ya Jumatano ijuma lijalo tarehe 29.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment