Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, January 25, 2014

Dk Slaa: Uswahiba wa JK, Kawambwa unaua elimu


Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa 
Na Raymond Kaminyonge, Mwananchi
Mbeya na Arusha. Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa amesema, uswahiba wa Rais Jakaya Kikwete na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa ndiyo chanzo cha kuporomoka kwa cha elimu nchini.
Dk Slaa alisema hayo jana kwenye Viwanja vya Jojo Kata ya Santilya, Mbeya Vijijini ikiwa ni siku ya tatu ya Operesheni la Vuguvugu la Mabadiliko (M4C), Pamoja Daima.
Alisema Dk Kawambwa hana uwezo wa kuongoza wizara hiyo muhimu kwa maendeleo ya taifa na Chadema kilishangazwa na mabadiliko aliyoyafanya Rais Kikwete katika baraza lake huku akimwacha waziri huyo katika nafasi hiyo.
“Kawambwa ni janga la elimu, hana uwezo. Chadema tutaendelea kumshtaki kwa wananchi. Mfumo mzima wa elimu nchini unahitaji mabadiliko, ili kufika huko wanahitajika viongozi wabunifu,” alisema Dk Slaa huku akishangiliwa na mamia ya wananchi waliohudhuria mkutano huo.
Aliongeza: “Elimu yetu iko shakani, sasa hivi mwenye shahada mbili anafanana na aliyemaliza darasa la nne la zamani.”
Alisema viongozi wa Serikali na CCM hawana uchungu kwa kuwa watoto wao wanasoma nje ya nchi hivyo aliwataka wananchi kuitosa CCM katika kila ngazi ya uchaguzi.
Dk Slaa alitumia nafasi hiyo kuwataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika baadaye mwaka huu.
Naye Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi maarufu kama ‘Sugu’ aliwataka wananchi hao kumchagua mgombea Udiwani wa Chadema, Elisha Mwandele katika uchaguzi mdogo wa Kata ya Santilya utakaofanyika mwezi ujao.
“Ninyi wananchi ndiyo wenye mamlaka kwa kila kitu, nawaombeni mumchangue Mwandele ili awe diwani wa kata hii na mabadiliko yataendelea nchi nzima ili tutume salamu kwa CCM,” alisema Mbilinyi.
Katika hatua nyingine, Helikopta ‘Chopa’ inayotumika katika ziara hiyo ililazimika kukaa kwa zaidi ya saa mbili katika uwanja wa Jojo kutokana na mvua na ukungu.
Kabla ya kufika hapo helikopta hiyo ilikuwa ikitokea Kyela mkoani humo na baadaye hali ya hewa iliporejea katika hali ya kawaida ziara iliendelea kwa Jimbo la Mbozi, kisha kuelekea katika Mkoa wa Katavi.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment