Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, January 25, 2014

Amng’ata meno mtoto baada ya kumfanyia ukatili mkewe


Picha ikimwonyesha mtoto Zakaria (1) na jeraha lake lililotokana na kung’atwa na baba yake. 
Na Anthony Mayunga, Mwananchi
Serengeti. Wakati alipoolewa kuwa mke wa pili kwa mahari ya ng’ombe wanane, Katarina Mturi (22) alisindikizwa kwa ngoma na tamaduni za Kabila la Kikurya, wala hakuamini kama kuna siku ataichukia ndoa hiyo.
Inawezekana hakuamini hivyo kwa kuwa mume wake Matata Makali (siyo jina halisi), ambaye alionekana mwenye upendo na kujali, pengine ni kwa sababu ya mapenzi mapya ya binti mdogo.
Katarina alikuwa ameolewa mara ya pili akitoka kwa mume wake wa kwanza aliyedai hakuwa na hata chembe ya upendo ndipo kwa kushauriana, familia yake ilimrudishia mahari mwanaume huyo na ndoa kuvunjika.
Mwanamke huyo anasema kuwa alikaa nyumbani kwao kwa muda, ndipo akajitokeza Matata(45), akiamini kuwa sasa amepata mume mwema.
Hata hivyo, hali ilikuwa kinyume, kwani leo Katarina ambaye ni mkazi wa Kitongoji cha Chinato, kijijini Bisarara, Kata ya Sedeco katika Wilaya ya Serengeti iliyopo Mkoa wa Mara, amekuwa miongoni mwa wanawake wanaosimulia ukatili wa kijinsia katika ndoa. Kutokana na yaliyomkuta, anaona kuwa ndoa siyo tena hitaji lake muhimu maishani.
Kwa nini?
Pamoja na mateso, kipigo alichokuwa akipata, alijitahidi kuvumilia familia yake ikimtia moyo na kumweleza kuwa ndoa ndivyo zilivyo.
Lakini Katarina anasema hatosahau tukio la saa 2:30 usiku, Januari 8 mwaka huu, ambapo mumewe huyo mpya alimfanyia ukatili bila kuwa na chembe ya huruma.
Katarina anaeleza kwamba hofu yake sasa ni ukatili kumwachia ulemavu.
“Katika hali ambayo mpaka leo sijaielewa, nilikuwa ndani na wanangu wawili, mkubwa na huyu mdogo mume wangu aliingia ndani akaniamuru niswage ng’ombe usiku huo kwenda ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kwa malisho. Nilikakataa, kwa sababu ilikuwa ni usiku. Nilimweleza kuwa kisheria haikubaliki kuchungia mifugo ndani ya Hifadhi ya Taifa, tena  kuna wanyama wakali na mimi ni mwanamke nitafanyaje?,” anasimulia.
Katarina anaongeza akionyesha maeneo aliyoumizwa: “Maneno hayo yakamkasirisha na kilichotokea ndiyo kama unavyoona.”
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment