Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Sunday, December 22, 2013

Rais Obama avionya vikosi vya uasi nchini Sudani Kusini

Rais wa Marekani Barack Obama .
Rais wa Marekani Barack Obama .

Na Sabina Chrispine Nabigambo
Rais wa Marekani Barack Obama jana Jumamosi amevionya vikosi vya waasi nchini Sudan Kusini dhidi ya mapinduzi ya kijeshi baada ya wanajeshi wanne wa Marekani kujeruhiwa katika shambulizi dhidi ya ndege yao wakati wakijielekeza mjini Bor kwa shughuli za uokozi.

Taarifa ya ikulu ya Marekani imeeleza kuwa juhudi zozote za kunyakua madaraka kwa nguvu za kijeshi zitasababisha kukoma kwa msaada wa muda mrefu kutoka Marekani jumuiya ya kimataifa.
Rais Obama amesisitiza kuwa viongozi wa Sudani Kusini wanalo jukumu la kusaidia juhudi za Marekani kuwaokoa wamarekani na raia huko Juba na Bor mji ambao unashikiliwa na waasi.
Onyo la rais Obama linakuja baada ya ndege tatu za Marekani kushambuliwa kwa risasi wakati zikielekea huko Bor kusaidia juhudi za kuwaondoa wa Marekani nchini Sudani Kusini kufuatia kuchacha kwa mapigano baina ya serikali na waasi.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment