Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, December 2, 2013

Hoja ya kumwondoa Waziri Mkuu Somalia


Bunge la Somalia limeanza kujadili hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu wa nchi hiyo Abdi Farah Shirdon ambaye amekuwa haelewani na rais wa nchi hiyo Hassan Sheikh Mahamud.
Waziri Mkuu wa Somalia Abdi Farah Shirdon
Bwana Shirdon hivi karibuni amekuwa akimkosoa rais wa nchi hiyo kwamba amekuwa akiongoza nchini hiyo bila kufuata katiba.
Wafuasi wa rais Hassan wanasema Waziri Mkuu huyo ameshindwa kutekeleza majukumu yake na uongozi wake umekuwa hauna mafanikio.
Mwandishi wa habari wa BBC aliyepo Somalia anasema mgawanyiko katika serikali ya Somalia iliyoundwa mwaka jana, unatishia juhudi za kuimarisha utulivu nchini humo baada ya nchi hiyo kuathirika na mgogoro kwa takrabani miongo miwili.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment