Writen by
sadataley
12:10 PM
-
0
Comments
Makundi ya kutea haki za Binaadam nchini Misri yamekosoa uamuzi wa mamlaka kuhukumu kifungo cha miaka kumi na mmoja dhidi ya kundi Waandamanaji wa kike kutoka chama cha kiislamu nchini humo.
Wanawake 21 na wasichana walikamatwa mwezi uliopita baada ya kutokea maandamano mjini Alexandria yaliyokuwa yakimuunga mkono Kiongozi aliyeondolewa madarakani, Mohamed Morsi , huku Familia moja ikidai binti wa familia hiyo alikamatwa alipokuwa akipita eneo lenye maandamano akielekea shuleni.
Walithibitishwa kuwa na makosa ya kutumia nguvu na hujuma, lakini washtakiwa walikana wakidai kuwa maandamano hayo yalikuwa ya amani.
Mwandishi wa BBC jijini Cairo amesema kuwa hukumu iliyotolewa imedaiwa kudhihirika kwa kuwepo kwa utawala wa mabavu nchini humo
No comments
Post a Comment