Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Wednesday, November 20, 2013

Ubalozi wa Iran washambuliwa Beirut

Watu wapatao 22 wameripotiwa kuuawa katika milipuko miwili ambayo imepiga mfululizo karibu na ubalozi wa Iran katika mji mkuu wa Lebanon, Beirut.
Mlipuko karibu na ubalozi wa Iran, mjini Beirut, Lebanon
Afisa ubalozi wa Iran Ebrahim Ansari ni miongoni mwa waliouawa katika milipuko hiyo. Maafisa wamesema idadi ya waliokufa inaweza kuongezeka.
Picha za televisheni zimeonyesha magari yakiungua, maiti zikiwa zimelala mtaani na majengo yaliyoharibiwa.
Iran imekuwa ikikiunga mkono kikundi cha Hezbollah ambacho ni cha wapiganaji wa madhehebu ya Kiislam ya Shia, ambacho kimetuma wapiganaji wake kwenda Syria kusaidia serikali ya Rais Bashar al-Assad.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment