Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, November 25, 2013

Meya wa Kampala afurushwa ofisini

Meya wa mji mkuu wa Uganda, Kampala, ameondolewa ofisini na madiwani baada ya jopo maalum kumpata na hatia ya matumizi mabaya ya mamlaka yake pamoja na kutokuwa na ujuzi wa kutosha kwa kazi yake.
Polisi walilazimika kutumia gesi ya kutoa machozi kuwatawanya wafuasi wa Lukwago
Erias Lukwago aliondolewa ofisini baada ya madiwani kupiga kura huku akipata kura tatun kati ya 29 zilizopigwa.
Polisi walilazimika kutumia gesi ya kutoa machozi kuvunja maandano ya wafuasi wa Lukwago.
Wafuasi wake wanaamini kuwa serikali ilipanga kumwondoa ofisini ili kuchukua wadhifa wa meya kutoka kwa upinzani.
Lukwago ni mwanachama wa chama cha upinzani cha Democratic Party (DP).
Alichaguliwa kama meya mwezi Januari mwaka 2011.
Wiki mbili zilizopita, serikali iliteua jopo lililomchunguza Lukwago na kuamua kuwa miongoni mwa makosa aliyoyafanya ni kukosa kuandaa mikutano muhimu , kupuuza wakuu waku wake na kuchochea umma kutolipa kodi.
Bwana Lukwago alitaja jopo hilo lililoongozwa na jaji kama, mahakama ya kipuuzi na kusema kuwa Rais Yoweri Museveni, ndiye aliyechochea jambo la kumwondoa ofisini ili washirika wake waweze kuchukua madaraka, baada ya kushindwa kwenye uchaguzi wa mwaka 2011.
Vurugu zilizuka na kutatiza usafiri mjini Kampala baada ya wafuasi wa Bwana Lukwago kupinga kuondolewa kwake ofisini.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment