Latest News

GNM Cargo

GNM Cargo
GNM CARGO & LOGISTICS

menu

Saturday, November 16, 2013

Kiza kinene: Dar, mikoa kibao kukumbwa na siku 10 za mgao wa umeme

Watanzania yabidi kuanza kutafuta mishumaa kabisa wakati wakijiandaa na machungu ya mgao mkali wa siku 10 uliotangazwa jana na Tanesco. PICHA | AFP 
Na Goodluck Eliona, Mwananchi
Dar es Salaam. Majiji yote matano nchini pamoja na Zanzibar na mikoa mingine kadhaa yatakuwa na giza kwa siku kumi kuanzia leo, hivyo kusababisha adha kwa wakazi wake. 
Meneja Uhusiano wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) Badra Masoud, amethibitisha kuwepo kwa adha hiyo, akielezea kuwa hali hiyo inatokana na kuzimwa kwa mitambo ya Kampuni ya Pan African iliyopo Songosongo.
“Mitambo hiyo itazimwa kwa sababu ya matengenezo ya lazima, hakuna jinsi ya kuzuia hali hiyo Tanesco tunasikitika sana kwa kuwa kutakuwa na upungufu mkubwa wa umeme kwenye gridi ya taifa,” alisema Masoud.
Alifafanua mitambo hiyo inaendeshwa na gesi ambayo imepungua katika kisiwa hicho cha Songosongo Wilaya ya Kilwa, Lindi. 
“Upungufu huo umesababishwa na matengenezo ya kiufundi yanayofanywa kwenye visima vya gesi, lengo ni kuboresha upatikanaji wa gesi ya kutosha kwenye visima hivyo,” alisema.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment