Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, November 29, 2013

JK auzindua Mkoa wa Simiyu

Rais Jakaya Kikwete.PICHA|MAKTABA 
Na Frederick Katulanda na Faustine Fabian, Mwananchi
Simiyu. Rais Jakaya Kikwete amezindua Mkoa mpya wa Simiyu na wilaya zake huku akisimikwa kuwa Mtemi wa Kisukuma na kupewa jina la MunguBhanu lenye maana ya Mungu watu.
  Katika uzinduzi  huo uliofanyika juzi jioni kwenye Uwanja wa Mashujaa wa Bariadi Mjini na kuahirishwa baada ya  mvua kunyesha, Rais alieleza kuwa lengo la Serikali katika uanzishaji mikoa hiyo na wilaya zake ni kusogeza huduma karibu na wananchi.
  Hata hivyo, sherehe hizo ziliendelea jana asubuhi ambapo Rais Kikwete alisimikwa kuwa Mtemi wa Kisukuma, shughuli zilizoambatana  na maombi ya kuomba baraka ya mvua, hekima, utajiri na neema kwa ushirikiano wa wazee wa jadi ambao ni watemi wa Kabila la Kisukuma mkoani humo.
Zoezi la kuuombea baraka Mkoa wa Simiyu pamoja na kuusimika kijadi, liliendeshwa na Watemi Charles Doto Itale wa Bujashi akiwa pamoja na Mtemi Andrew Chenge (Itilima) Mbunge wa Bariadi Mashariki, Wenseslaus Seni (Kanadi), John Ngemela (Magu) waliomvisha joho na kumkabidhi Utemi  Rais Kikwete.
Mkoa wa Simiyu ulianzishwa rasmi mwaka jana na kuwa mkoa wa nne kati ya mikoa iliyogawanywa katika maeneo mbalimbali ikiwamo mikoa ya  Geita, Njombe pamoja na Katavi hivyo kuifanya Kanda ya Ziwa kuwa na jumla ya mikoa sita.
Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Hawa Ghasia alieleza kuwa Serikali imetenga Sh17 bilioni kwa ajili ya mkoa huo fedha ambazo amedaiwa ni kwa ajili ya kujenga miundombinu pamoja na nyumba za watumishi hivyo alitoa wito wa matumizi yaliyokusudiwa.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment