Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Sunday, July 21, 2013

Mapendekezo ya (CCM) kuhusu Rasimu ya Katiba Mpya


                                                                                   Nape Nnauye 
Na Mwandishi Wetu
Mapendekezo ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuhusu Rasimu ya Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa wanachama na viongozi wake.
UTANGULIZI
1.1 Mnamo tarehe 03/06/2013 Tume ya Mabadiliko ya Katiba ilitangaza rasimu ya kwanza ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
1.2 Rasimu hii ya Katiba itajadiliwa katika mfumo wa aina mbili wa mabaraza:
Mabaraza ya Katiba ya Wilaya, ambayo yameshaundwa na yatatoa maoni yake kupitia mikutano itakayoitishwa na Tume ya Marekebisho ya Katiba. Mabaraza haya yanasimamiwa na Tume yenyewe.
Mabaraza ya Asasi, Taasisi na makundi ya watu wenye malengo yanayofanana kama vile vyama vya siasa na jumuiya za kidini na kadhalika. Mabaraza haya yanasimamiwa na Asasi au Taasisi husika.
1.3 Chama Cha Mapinduzi kimeshajiunda kama Baraza la Katiba la kitaasisi na kutambuliwa rasmi na Tume kwa barua Kumb.na. AB 76/386/57 ya tarehe 24/052013
1.4 Kwa kuzingatia kwamba Chama Cha Mapinduzi ni Taasisi muhimu na yenye masilahi makubwa katika upatikanaji wa Katiba Mpya, Kamati Kuu ya Halmashauri ya Taifa iliyokutana mjini Dodoma Tarehe, 10/6/2013, pamoja na mambo mengine ilielekeza kwamba uandaliwe utaratibu utakaohusisha utoaji wa maoni utakaotumiwa na wanaCCM kutoa maoni yao.
1.5 Madhumuni ya ufafanuzi huu ni kujenga uelewa wa pamoja wa maudhui ya Rasimu ya Kwanza na hivyo kuwawezesha wanaCCM kushiriki kutoa maoni yao kikamilifu kutoka ngazi ya matawi hadi taifa.
UTARATIBU WA KUTOA MAONI
2.1 Kwa upande wa matawi maoni yatatolewa kupitia mikutano
Kwa wilaya, mikoa na taifa. Maoni yatatolewa kupita halmashauri kuu zao.2.2 Ili kupata mfumo wa aina moja wa kuijadili Rasimu ya kwanza na kutoa maoni, wanachama wanaelekezwa kuzingatia vigezo vifuatavyo:
Kuitaja sura ya Rasimu ya Katiba inayohusika
Kutaja ibara ya Rasimu ya Katiba
Kutoa maelezo juu ya Ibara hiyo (kama kuna upungufu au maoni mengine yoyote);
Mapendekezo ya marekebisho
Sababu za mapendekezo ya marekebisho hayo.
MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA
3.1 Ieleweke kwamba hii ni rasimu ya kwanza ya Katiba na siyo Katiba rasmi au iliyokamilika. Baada ya maoni ya mabaraza ya Katiba ya Wilaya na kitaasisi itafuata rasimu ya pili itakayowasilishwa kwenye Bunge la Katiba. Mwisho kutakuwa na rasimu ya tatu itakayofikishwa kwa wananchi kwa ajili ya kupigiwa kura ya maoni yao kwa uhuru na kwa kina.
3.2 Kwa mujibu wa mwongozo wa Tume, Wajumbe wa Mabaraza ya Wilaya wanaweza pia kushiriki kama Wajumbe wa Mabaraza ya Katiba ya asasi au Taasisi ili mradi ni mwanachama wa Asasi au Taasisi husika. Kwa mantiki hii wanaCCM walioko kwenye mabaraza ya katiba ya wilaya wanahimizwa kushiriki kikamilifu kwenye ngazi husika za Mabaraza ya Katiba ya CCM kama taasisi.
3.3 Maoni yatakayotolewa kupitia mabaraza ya katiba yanatakiwa yawe yameifikia Tume ya Marekebisho ya Katiba kabla au ifikapo Agosti 31, 2013.
3.4 Katika awamu ya kwanza ya mchakato wa kutoa maoni Chama Cha Mapinduzi kiliandaa mwongozo wake uliojielekeza kwenye mambo makuu ya msingi na yenye masilahi ya pekee kwa Taifa letu.
3.5 Vivyohivyo katika kipindi hiki cha kutoa maoni juu ya Rasimu ya Kwanza, Chama Cha Mapinduzi kinawaelekeza wana-CCM kujadili kwa umakini maeneo hayo na kwa masilahi ya Taifa letu.
Chanzo: www.mwananchi.co.tz
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment