UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

Wednesday, April 18, 2018

DRC kukabidhi kwa Rwanda askari iliowakamata

Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo limesema kuwa, askari wa Rwanda waliokamatwa mwishoni mwa juma lililopita katika mkoa wa Kivu Kaskazini watakabidhiwa mamlaka husika ili waweze kurejeshwa nchini Rwanda.
Kwa mujibu wa duru za habari, askari wawili wa Rwanda walikamatwa na silaha na vifaa vya mawasiliano usiku wa Jumapili kuamkia Jumatatu karibu na uwanja wa ndege wa Goma mashariki mwa Jamhuri yya Kidemokrasia ya Congo.


Meja Guillaume Ndjike, mmoja wa wasemaji wa jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo katika mkoa wa Kivu Kaskazini

Kwa mujibu wa Meja Guillaume Ndjike, mmoja wa wasemaji wa jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo katika mkoa wa Kivu Kaskazini, askari hao wa Rwanda watakabidhiwa kwa tume ya pamoja yenye dhamana ya kukagua mipaka kati ya nchi hizo mbili.
Taasisi hii itahusika na kukabidhi askari hawa kwa serikali ya Rwanda, amesema msemaji huyo wa jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo

Meja Ndjike aidha  ameiomba nchi jirani ya Rwanda nayo kutumia utaratibu huo wakati askari wake wanapokuwa kwenye ardhi yake.
Kumekuwa na mvutano kwa miaka kadhaa kati ya Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ambapo Kinshasa imekuwa ikimtuhumu jirani yake huyo kwamba, amekuwa akisaidia makundi ya watu wenye silaha nchini humo. 
Hata hivyo serikali yya Kkigali imekuwa ikkikanusha tuhuma hizo na kusisitiza kwamba, haihusikki kwa namna yoyote na machafuko yanayoendelea mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Parstoday
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment